Jumatano, 4 Januari 2017



CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU CHA DAR ES SALAAM  (DUCE)
KITIVO CHA HUMANITIA NA SAYANSI JAMII
IDARA YA  ISIMU NA LUGHA.

KOZI:                                       FASIHI ANDISHI YA KISWAHILI
MSIMBO WA KOZI:                  KF 202
KIONGOZI WA SEMINA:          MADAM GRACE
WASHIRIKI
NA
JINA KAMILI
NAMBA
PROGRAMU
SAHIHI
1
KIFYASI ONJENI WILLIUM
2014-04-05422
BAED

2
PASIANI EDINESTA INYASI
2014-04-05206
BAED

3
MLIMAKIFI HANZISTIN M
2014-04-05700
BAED

4
MWAZINI MIGISHA AUGUSTINO
2013-04-07105
BAED

5
KIDAVA SAYUNI NEHEMIA
2014-04-05428
BAED

6
SALIMU MONICA
2014-04-08120
BAED

7
YUNGE ISMAIL NKALI
2014-04-05722
BAED

8
SULLE VERONICA P
2014-04-05645
BAED

9
SERIKALI PILI
2014-04-07924
BAED

10
DAWSON EPIMARK
2014-04-07948
BAED


INSHA YA MUHULA.
                               “Suala la majaribio na mabadiliko katika fasihi andishi ya Kiswahili halikwepeki”. Jadili kauli hii kwa kutumia kazi mbalimbali za fasihi andishi ya Kiswahili



MPANGO KAZI
UTANGULIZI
Ø  Maana ya fasihi andishi.
Ø  Maana ya fasihi andishi ya Kiswahili.
KIINI
Ø  Mabadiliko na majaribio katika tamthiliya, Tiwaya, Hadithi fupi na Ushairi.
HITIMISHO

MAREJELEO





Maana ya fasihi andishi imetolewa na wataalamu mbalimbali, kwa mujibu wa Wamitila (2003), ni sanaa itumiayo maandishi kufikisha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa, pia anasema fasihi andishi ina tanzu mbalimbali kama vile Riwaya, Tamthiliya na Ushairi. Kwa mujibu wa www.shuledirect.co.tz/notes  wanasema fasihi andishi ni tawi la fasihi linalo tumia sanaa ya maneno kufikisha ujumbe kwa hadhira kwa njia ya maandishi, zipo aina nyingi za fasihi andishi miongoni mwa hizo ni pamoja na Ushairi, Riwaya, Hadithi fupi na Tamthiliya. Kwa ujumla tunasema fasihi andishi ni aina ya sanaa ambayo hutumia maneno yaliyoandikwa ili kufikisha ujumbe kwa hadhiira iliyokusudiwa. Fasihi andishi ya Kiswahili kwa mujibu wa Mulokozi (1996) akiwanukuu Syambo na Mazrui (1992) fasihi andishi ya Kiswahili ni fasihi iliyoandikwa kwa Kiswahili tu, iwapo inazungumzia utamaduni wa Kiswahili au utamaduni mwingineo. Maadam fasihi hiyo imetumia lugha ya Kiswahili na imefuata mbinu za ufasaha wa lugha hiyo basi kwa tafsiri yao ni fasihi ya Kiswahili. Kwa ujumla fasihi andishi ya Kiswahili ni sanaa ya lugha iliyotungwa kwa lugha ya Kiswahili na kuwasilishwa kwa hadhira (msomaji) kwa njia ya maandishi yenye kuelezea utamaduni wa jadi ya Kiswahili. Hivyo basi zipo aina nne za fasihi andishi ya Kiswahili kama vile Riwaya, Ushairi, Tamthiliya na Hadithi fupi. Kwahiyo ni kweli suala la mabadiliko na majaribio katika fasihi andishi ya Kiswahili halikwepeki kutokana na mabadiliko yanayotokea katika jamii ya Kiswahili kama ifuatavyo;
          Riwaya, Wamitila (2003) anasema kuwa ni kazi ya kinathari au kibunilizi ambayo huwa na urefu wa kutosha, msuko uliojengeka vizuri, wahusika wengi walioendelezwa kwa kina, yenye kuchukua muda mwingi katika maandalizi na kuhusisha mandhari maalumu. Muhando na Balisidya (1976) wanaeleza riwaya ni kazi ya kubuni, ni hadithi ambayo hutungwa kufuatana na uwezo wa fanani kuibusha mambo kutokana na mazoea au mazingira yake. Hivyo basi riwaya ni hadithi ndefu ya kubuni yenye mawanda mapana, lugha ya kinathari, mchanganyiko wa visa na dhamira yenye kufungamana na wakati na kushabihiana na maisha halisi na riwaya huwa na sifa kama vile masimulizi ya kubuni, usimulizi wa kinathari, mpangilio wa msuko wa matukio, hufungamana na wakati, urefu wakuanzia maneno 35000 na kuendelea na iwe na mawanda mapana.
          Fasihi huithamini jamii kiitikadi, kisiasa, kiutamaduni, kiuchumi na kijamii. Imekuwa ikibadilika badilika kimtazamo fasihi nayo imekuwa ikibadilika kwasababu jamii nayo inabadilika. Mabadiliko hayo katika riwaya (fasihi) kutokea kwasababu ya wasanii kutumia vionjo vipya katika kuiumba kazi hiyo kama anavyosema Khamis (2007)  mara moja tunaona neno kionjo linajisemelea lenyewe kimya kimya juu ya mabadiliko ya utanzu wa fasihi. Mabadilko yaliyotokea katika utanzu wa riwaya ni kama yafuatayo;
          Kabla ya ukoloni, sehemu kubwa ya riwaya ya Kiswahili ilikuwa ya kisimulizi (ngano, hekaya na tendi) baadhi ya tendi hizo ni “Siri Asirari” (Binti Temba 1863), “Kawaida ya Hamzia” (1652) huu ulikuwa ni utenzi uliomsimfu mtume Muhhamed ulitungwa na Mwarabu aitwaye Ali Hamzia. Katika kuandika riwaya za mwanzo waliweka misingi na mitindo inayofuatwa na watunzi wa leo.
          Wakati wa ukoloni, wakati wa utawala wa Waingereza 1930 baada ya kuanzishwa shirika la uchapishaji la Afrika Mashariki, East Africa Literature Bureau (EALB) shirika hili liliwahimiza Waafrika kuandika vitabu kwa lugha ya Kiswahili na kuchapisha. Kipindi hiki kulikuwa na mashindano ya uandishi wa riwaya za Kiswahili kutokana na mashindano hayo waandishi wengi waliibuka na riwaya ya kwanza ya Kiswahili iliitwa “Uhuru wa Watumwa” iliandikwa na James Mbotela 1885 na kilichapishwa 1934, “Mzimu wa Kale”  S. Abdallah 1960, “Simu ya Kifo”  F. Katambula 1963. Riwaya zote hizo zilichapishwa na shirika la uchapishaji la Afrika Mashariki (EALB) Riwaya za wakati huo zilizungumzia kuhusu athari ya biashara ya utumwa na namna ya kujikomboa na mfumo wa ukoloni na maadili mema.
          Wakati wa uhuru (1961 hadi 1967), Riwaya nyingi zilijadili juu ya ujenzi wa jamii mpya, madhara ya unyonyaji, matabaka, athari za azimio la Arusha pamoja ba umuhimu wa elimu. Mfano wa riwaya hizo ni kama vile “Dunia Uwanja wa Fujo” ( E. Kezilahabi), “Njozi Iliyopotea” Mung’ong’o miaka ya 1967-1980. Riwaya nyingi zilieleza kuhusu  umuhimu wa kuishi vijijini, madhara ya vita, hali ngumu ya maisha, madhara ya ujamaa na unafiki wa viongozi wetu mfano. “Miradi Bubu ya Wazalendo (E. Ruhumbika), “Shida”, “Nyota ya Rehema”, “Kiu ya Haki”.
          Kipindi cha 1980 hadi sasa, ni Riwaya zinazojadili madhara ya rushwa, mapenzi, ndoa, matokeo ya ukoloni mamboleo pamoja na mfumo wa kidemokrasia, mfano. “Mfadhili"  (Hussein Tuwa), “Vuta N’kuvute” (Shaffi A. shaffi) na “Usiku Utakapokwisha” (Mbunda Msokile).
          Utanzu mwingine ni Ushairi. Ushairi umeelezwa na wataalamu mbalimbali wakitoa maana ya ushairi kama  Amri (1954) ushairi au utenzi ni wimbo hivyo anasema kama shairi haliimbiki halina maana. Shaaban Robert (1956) ushairi ni sanaa ya vina inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tendi au tenzi. Kezilahabi (1976) anasema kuwa ushairi ni tukio/ hali au wazo ambalo limeoneshwa kwetu kutokana na upangaji mzuri wa maneno ya fasihi yenye mizani au uizani kwa ufupi ili kuonesha ukweli Fulani wa maisha. Hivyobasi tunaweza kusema kuwa ushairi ni sanaa ya lugha ya mkato inayosawili, kueleza au kuonesha jambo, kuonesha hisi, au hali ya namna ya kuvutia katika mpangilio mahususi wa maneno wenye urari wa uizani (mizani) wa sauti. Majaribio na mabadiliko katika ushairi wa Kiswahili yanafafanuliwa na Wangai Mwai (2008:73) anasema fasihi hubadilika badilika katika kumbo na maudhui kwahiyo ushairi wa Kiswahili sharti uruhusu mabadiliko yanapotokea hivyo dunia inapobadilika na ushairi hauna budi kubadilika, mabadiliko hayo yalitokea katika vipindi vifuatavyo kwa mujibu wa Kezilahabi 1983;
          Muhula wa urasimu (0 hadi 1885) katika muhula huu kanuni za utunzi wa ushairi ziliwekwa na zilitawaliwa na mitazamo ya kidini na mamwinyi. Mfano kulikuwa na tendi nyingi zilizo ibuka huko Arabuni wakati wa mtume Muhhamad mfano. “Shutaki Anganwa”,Nakaa”, “Masahibu” pia kulikuwa na tungo za kitamaduni, mawaidha na tumbuizo mfano. “Utendi wa Mwanakupona” katika kipindi hiki pia kulikuwa na utawala wa kiarabu, kilitawaliwa na fasihi ya kidini ambayo ilitafakari theolojia na tafakari ya maisha.
           Muhula wa utasa (1885 hadi 1945) katika muhula huu ulikuwa wakati wamabaliko ya kiutawala, kielimu na kiuchumi. Hivyo mashairi machache tu yalitungwa. Pia mabadiliko kutoka hati ya kiarabu kwenda ya kirumi. Maandishi yaliyoandikwa yalikuwa ya Hemed Abdallah, Baadhi ya tenzi zinazopatikana ni “Utenzi wa Vita vya Majimaji” .Kanuni za uiandishi wa mashairi zilianza kupotea.
          Muhula wa urasimu mpya (1945 hadi 1965) hiki kilikuwa kipindi cha kufufua kanuni za utunzi. Shaban Robert, Amri Abed, Khamis Aman na watalaamu wengine waliibua kanuni hizo za utunzi wa ushairi. kipindi hiki ndipo kitabu cha kutunga mashairi kiliandikwa wakati ambapo kilikuwa kinahitajika sana ilikuweka kiungo kizuri na wakati ulipo (1954) mtindo uliotumika sana ni ule wa mizani 16, yaani nane kipande cha kwanza na nane kipande cha pili ,
          Muhula wa sasa (1960 hadi sasa) Ni muhula wa kimutazamo mpya wa kimawazo na kisanaa. Hivyo kuna mgogoro katika uwanja wa ushairi, Kati ya washairi wanaofuata uhuru wa kisanaa. Hivyo mgogoro huu ulikuwa baina ya wanausasa na wanamapokeo ambapo baadhi ya wanausasa ni kama Kezilahabi, M.M Mulokozi K.K Kahigi walianza kuandika kazi za ushairi zisizo kuwa na urari wa vina na mizani. Wengi walichukulia kushusha maendeleo ya ushairi lakini wanausasa waliona ni hatua ya maendeleo. Hivyo mashairi yalitungwa kwa mfumo huo yaliapata majina kam vile Makue, Mtiririko na Mapingiti.
          Ibrahim Noor Shariff (1988:183) Amedai kuwa mzozo uliibuka pale wanamabadiliko walipodai mambo matatu (3): Mbinu za kutunga mashairi zilikuwa chache mno, sheria za kutunga mashairi ziliwanyima uhuru watunzi kutunga na muundo wa tungo za kishairi ulikuwa wa Kiswahili hapo zamani haukuwa na vina wa mizani. Hivyo sheria si za lazima. Kauli hizi za wanamabadiliko zilipingwa sana na wanamapokeo ambao waliamini urari wa vina na mizani ndiyo roho ya ushairi.  Ruwaza ya vina na mizani ndizo znafanya ushairi wa Kiswahili ujitambulishe. Njogu na Chimela (1999:113) wanadai kwamba mgogoro huu ulikuwa kati ya vijana na wazee waliokuwa wamekulia katika mazingira ya tungo za vina na mizani.
          Tamthiliya (Wamitila 2002:7); Anasema tamthiliya ni utungo unaoandikwa kwa mazungumzo, ambacho ni kipengele muhimu katika tamthiliya. Mulokozi (1999) Anasema kuwa tamthiliya au drama ni fani ya fasihi iliyokusudiwa kutendwa jukwaani kwa ajili ya hadhira fulani. Ubora unaopatikana katika maana hii ni kuwa imezingatia utendwaji jukwaa, hadhira, kusudio, na fani iliyotendwa. Kwa ujumla, Tamthiliya ni utanzu wa fasihi unaotumia lugha ya majibizano nyenye ubunifu wa hali ya juu ikiwa haina msisitizo wa uwasilishaji wake jukwaani ili kufikisha lengo mahususi kwa hadhira iliyokusudiwa kwa njia ya kuandikwa au isiyo ya kuandikwa. Sifa za tamthiliya ni kama vile dhana inayotendwa, uwanja wa kutendea kazi, watendaji, hadhira, kusudio la kisanaa, muktadha wa kisanaa na ubunifu. Mabadiliko yanayotokea kwenye utanzu wa tamthiliya na kama ifuaytavyo;
          Kabla ya ukoloni; tamthiliya ziliandikwa ili ziigizwe jukwaani, hazikuwepo badala yake zilikuwepo ambazo hazikuandikwa bali za kuigizwa kwenye shughuli mbalimbali kama vile jando na unyago, mazishi, kwa mtemi,  harusi na michezo ya watoto. Sifa za tamthiliya hizo ni masimulizi (hadithi), wahusika, vitendo (utambaji), daiolojia. Hata hivyo tamthiliya hizo hazikuwa na ki- Aristotle, wala hazikuwa na matini zilizoandikwa, hivyo zilikuwa tamthiliya simulizi.
          Kipindi cha ukoloni. Kipindi hiki kilianza mwaka (1890 hadi 1960) hapa palikuwa na aina kuu mbili za tamthiliya zisizo za kijadi. Tamthiliya za kizungu na vichekesho, mwishoni mwa kipindi hiki palitokea aina nyingine ya tamthiliya ya kiswahili iliyoitwa tamthiliya ya Kiswahili 1950. Aina hizi zimefafanuliwa kama ifuatavyo;
          Tamthiliya za kizungu, Hizi zilikusudiwa kuwaburudisha maofisa wa kizungu kama maseneta, kufundisha biblia na kueneza imani ya kidini. Tamthiliya nyingi ziliandikwa kwa lugha ya kiingereza na ziliigizwa shuleni, kiribu ya tamthiliya za kipindi hicho zilikuwa za kibwenyenye (maisha ya starehe) tamthiliya chache sana ziliandikwa kwa Kiswahili mfano , ‘Tabibu Asiyependa Utabibu’  kimeandikwa na A. Marrison. Vikundi vingi vilianzishwa kwa ajili ya kuigiza tamthiliya ya kizungu mfano Dar es Salaam players (little theatre) 1947 na Arusha little theatre Musuka 1953.
Vichekesho; Ni aina ya  tamthiliya geuzwa yaani hutungwa papo kwa papo bila kuandikwa.  Tamthiliya hizi zilianza miaka ya 1920 kwa lengo la kuburudisha wenyeji. Tamthiliya nyingi zilikuwa na vituko vya kuchekesha na zilijenga kuigiza kuhusu ushamba, ujinga na kutokuwa  msitaarabu. Tamthiliya hizi zilimuonesha  mhusika anaetoka shamba na kwenda kuzurula mjini kutafuta kazi. Ziliendelea mpaka baada ya uhuru ila hivi sasa maudhui yake yamebadilika.
Tamthiliya andishi ya Kiswahili; hizi ziliandikwa kabla ya kuigizwa jukwaani na zilianza kutokea miaka ya (1950). Mfano Imekwisha ya      C.Frank,(1951), Tamthiliya nyingi za kidini zilindikwa mashuleni na kanisani tu lakini hazikuchapishwa vitabuni. Mfano Karibu  Mgeni ya Graham Hyslop (1957). Pia mwaka huo aliandaka kitabu cha Afadhari Mchawi, Nakupenda  Lakini…. ya Henry Kuria (1954), Nimelogwa nisiwe na Mpenzi ya Gerishon Ngugi (1961). kwa ujumla hadi tunapata uhuru tamthiliya zilikuwa zimeandikwa na Wakenya.
Kipindi cha uhuru hadi sasa; Tamthiliya ya kizungu iliendelea kuigizwa mashuleni na katika kumbi maalumu za maonyesho (Little theatres)baadhi ya tamthiliya maarufu zilitafsiriwa na kuigizwa ni za Julius Kaizali (Shakespear),Mabepari wa Venis ya JK. Nyerere(1969),Mfalume Edipode , Mchuuzi muungwana, Pia tamthiliya za Kiafrika zilizo tafsiriwa na kama Mtawa mweusi(The black Hermit)ya Ngugi wa Thiongo ,Nitaolewa Nikipenda (I will Merry when I want) ya Ngugi wa Thiongo na Ngugi wa Mini (1982). Kipindi hiki  kimegawanyika katika vipengele viwili ambavyo vimefafanuliwa kama ifuatavyo;
Vichekesho;  vichekesho viliwasuta wazungu weusi wanaoishi maisha ya kizungu, waliolingia elimu na vyeo vyao na kudharau wengine,Vilevile  vilijadili matatizo ya kijamii, ukosefu wa kazi, Ukimwi, Uhalifu, udanganyifu wa waganga wa kienyeji. Pia kulikuwa na vichekesho vya kisiasa ,ujamaa na ubinafsi wa viongozi ambao ambao sasa umetawala na Mtatizo ya kuanzishwa kwa vijiji vya ujamaa. Mfano kipindi cha Mahoka kilianzishwa mwaka (1974) Pwagu na Pwaguzi. Walikuwa wanachekesha Redio Tanzania vilikejeli baadhi ya tabia za viongozi na sera za Azimio la Arusha
Tamthiliya andishi ya Kiswahili; utanzu huu ulichochewa zaidi na mashindano yailiyoongozwa na chama cha waigizaji wa vijana Tanzania. Watanzania wengi walianza kuandika  tamthiliya za Kiswahili. Mfano “Wakati Ukuta”ya Ibrahim Hussein(1969). Tamthiliya hii ilishinda mashindano na kupewa tuzo, Kinjekitile ya Ibrahim Hussein (1969), pia Kaptula la Marx ya E.Kezilahabi. Tamthiliya andishi ya Kiswahili ilikuwa na maudhui ambayo twaweza kugawa tamthiliya ya Kiswahili kutoka mwaka 1960 hadi sasa kama vile;
Tamthiliya zinazoelezea migogoro ya utamaduni kati ya ukale na usasa, Mfano Nimelogwa nisiwe na Mpenzi ya Ngugi Gerishoni. Pia matatizo ya kijamii kama mapenzi, ndoa, ufukara na Urithi. Mfano Mke Mwenza, Nakupenda Lakini…, pia kuna tamthiliya za kidini zinazoelezea matatizo ya kidini zilizo ingia moja kwa moja toka ulaya. Mfano Aliyeonja Pepo ya F.Topari, ukombozi wa kitaifa hizi ni tamthiliya zinazoonesha harakati za ukombozi wa ukoloni pamoja na ukombozi wa Nyanja zote za maisha. Mfano Tone la Mwisho ya Emmanel Mbogo. Na mwisho walilenga ujenzi wa jamii mpya, Mfano Giza limeingia  ya Emmanuel Mbogo na Kijiji chetu  ya Ngaliyoma.
Hadithi fupi; Kwa mujibu wa Wamitila (2002:68) Hadithi fupi ni utungo mfupi wakinathari unaojishughilisha na suala fulani kuu, wenye wahusika ambao hawakuzwi, Na unaoutumia mbinu  za kimaelezo za kibunifu, zenye uelekezi wa kiwango cha juu. Kwa mujibu wa Msukile(1992), Ni aina ya kazi ya sanaa ya utanzu wa hadithi inayotumia  lugha iliyoandikwa kinathari au iliyo katika masimulizi kama haijaandikwa. Kwa ujumla hadithi fupi andishi ya Kiswahili; Ni aina ya kazi andishi ambayo huwa fupi na huangazia wazo moja  na kurejea kisa kimoja, Pia huwa na wahusika wachache na huchukua muda mfupi, hadithi fupi huwa na sifa kama vile kuwa na  athari za aina moja, urefu  wa kusomeka kwa mkao mmoja na itumie lugha iliiweze kuleta mguso wa kihisia na si kiakili.
Hadithi fupi andishi ya Kiswahili inabainishwa na Brander Methew anaye aminika kutumika neno la kiingereza Short story na kuonesha yeye nimiongoni mwawaasisi wa utanzu wa utanzu huu wa fasihi. Chimbuko la hadithi fupi ni masimulizi ya kijadi ambayo yanahusisha ngano, hekaya tendi na rara. Pia hadithi fupi andishi ya Kiswahili imetokana na hadithi fupi za kigeni. Mabadiliko na majaribio hayo yamejitokeza katika  vipindi vifuatavyo:
Miaka ya (1960) hadi (1970); kipindi hiki hadithi fupi ziliandikwa magazetini, Mfano gazeti la Mzalendo, Kiongozi, Mamboleo, Nchi nyetu na gazeti la Afrika Mashariki. Pia kipindi hiki mashindoni ya kuandika  hadithi fupi andishi yaliandaliwa. Miongoni mwake ni Chamnyonge utakipata Hadharani, Mayai Waziri wa Maradhi. Hatimaye zikaanza kusemwa redioni, mfano shirika la utangazaji la Britsh Broadcasting Cooperation (BBC). Baadaye zikaandikwa vitabuni ikiwa nimfululizo wa vitabu mbalimbali, mfano Pavumapo palilie na Kimya jumba la Maneno.
Miaka ya (1970) hadi (1980); katika kipindi hiki waandishi wengi walijitokeza  kuandika hadithi fupi mbalimbali, mfano Nitakuja kwa Siri na Kimya jumba la Maneno .
Miaka ya (1990), kipindi hiki hadithi fupi za Kiswahili zilidumaa kwa sababu waandishi wengi waliandika hadithi zenye dhamira za kufanana na wasomaji wengi walipuuza kwasababu hadithi nyingi ziliingiliana.
          Miaka ya ( 2000) hadi sasa;  Jitihada za uaindishi wa hadithi fupi zilianza tena na vitabu vingi viliandikwa na kukusanywa, hii ilitokana na mabadiliko ya utandawazi waandishi wengi walianza kuandika athari za utandawazi, mfano kitabu cha Mwendawazimu cha Mbatia, Mayai Waziri wa Maradhi na hadithi nyingine katika kitabu cha Wamitila.
          Hivyo basi fasihia andishi ya Kiswahili hubadilika kutokana na mabadiliko katka jamii. Hivyo kuna sababu ambazo hupelekea mabadiliko haya kama vile ugunduzi wa teknolojia ya upigaji chapa wa vitabu, ukuaji wa shughuli za kiuchumi, mageuzi ya kijamii na kisiasa yaliyofungamana na mabadiliko ya kiuchumi na sababu nyinginezo ndizo zilizosaidia kuleta mageuzi makubwa katika kazi ya Fasihi andishi ya Kiswahili.








                               


                                                  MAREJELEO
Abedi, A. (1954) Sheria za Kutunga Mashairi na Diwani ya Amri. Nairobi: EALB
                                       Chawakamamnma. Blogspot.com
Msokile, M. (1992). Misingi ya Hadithi Fupi, Dar es salaam: Dar es salaam                                                                                    University Press.
 Muhando, P na Balisidya, M. (1976) Fasihi na Sanaa za Maonesho. Dar es                                                       salaam: TPH
 Mulokozi, M,M. (1996),  Utangulizi wa Fasihi ya Kiswahili. Dar es salaam:                                              Chuo           Kikuu Huria, (ukur 1-93, 229-230).
Samwel, M & Akech, J (2013) Diwani ya MEA. Moveli publishers: Dar es                                                  Salaam.

               

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Matokeo kidato Cha pilibofya hapa

 KUTAZAMA BOFYA HAPA <https://matokeo.necta.go.tz/ftna2020/ftna.htm>